
SIMULIZI: MAMA YANGU ANAKULA NYAMA ZA WATU.. SEHEMU YA PILI
Baada ya Amina kufariki pale hospitali. Maiti ilichukuliwa na kurejeshwa nyumbani, ndani ya muda mfupi vilio vilitanda eneo lile lanyumbani kwakina Amina. Haikuchukua muda shughuli za mazishi zilianza, majira ya sasa kumi jioni marehemu Amina alikuwa teyari keshawekwa kwenye makazi yake ya milele. Ilikuwa gumzo kwa wengi wao maana kilikuwa kifo cha ghafla, hawakuhitaji kudadisi zaidi waliliacha swala hilo kama lilivyo kwakuamini nimipango ya Mungu. Baada ya mazishi watu wote walisambaratika nakuendelea na shughuli zao.
Siku ya 3 baada ya mazishi, Ulipo ingiausiku mnene jiji lilikua limepoa kwapirika za watu. Ndipo B.fatma(mama yake Nasibu) alikurupuka toka usingizini kisha akaelekea kwenye pembe ya chumba, nibaada ya kuvuu nguo zote nakubakia mtupu kama alivyo zaliwa. Kisha kutoweka kimazingara nakutokea mbuyuni, ambapo aliwakuta wenzake wakiwa wana msubiri yeyetu. Bilakupoteza muda, wote walikusanyana nakuelekea makaburini. Walipo wasili maeneo yale ya makaburini, walili zunguka kaburi la Amina huku wanaimba nyimbo zao za kichawi, wakatihuo kiongozi wao akiendelea kuufufua mwili wa Amina. Haikuwa kazi rahisi japokua muda mfupi walifanikiwa kuutoa mwiliule wa marehemu Amina.
Walirudi namwiliule hadi mbuyuni, kisha kuulaza chali juu ya ardhi baada ya kuufungua sanda yake.
Kiongozi mkuu, alisimama kisha kuitanga ziahadhira yake."hii ni kafara ya b.fatma kwa mizimu. kulinganana ahadi aliyoiweka miaka 20 iliyopita baada ya kushindwa kumtota kafara mwanaye Nasibu nahivyo analazimika kutoa wajukuu zake wawili tukianza nahuyu." baada ya hapo alianza kuucharanga charanga mwiliule bilahuruma, kisha kugawana mapande ya nyama ambayo hanyakuwa na damu kutokana ilisha nyonywa na mizimu. Baada yakula yamazile mbichi B.fatma yeye alikabidhiwa kichwa akakifukie nyuma ya nyumba yake, akiwa nimwenye kutetemeka alikipokea kichwakile. Nandipo wote walisambaratika kuelekea makwao. Muda ulikuwa umeenda sana ndipo b.fatma aliamua
Kulingana na muda ulikuwa umeenda sana B.fatma aliamua kukiweka kichwa kile chini ya uvungu wa kitanda chake.
Asubuhi kumepambazuka, watu walielekea kwenye shughuli zao za kilasiku. Mkewe Nasibu(Madsam) alikuwa kitandani akiwaza hili na lile mara ikamjia taswira ya marehemu mwanaye Amina, ambapo aliyakumbuka maneno aliyosema mwanae enzi za uhaiwake hukuakinung'unika "bibi...bibi...bibi..ananimaliza" Madsam alishituka kamamtu aliye kurupushwa toka usingizini, mapigo ya moyo yalimuendambiyo akanzakuwa na wasiwasi na mkwewe b.fatma juu ya kifo cha mwanaye Amina. Akalipunza jambo hili kwamuda nakisha kuendelea na shughuli zingine.
Jioni watu wanarejea toka kwenye mihangaiko yakimaisha. Nasibu na mkewe wakiwa chumbani wanabadilishana mawazo, Madsam alimgusia suala lile juu ya mashaka aliyonayo kwa mama yake, ilikuwa tofauti kwaupande wa Nasibu hivyo alimkemea na kumkaripia mkewe, ingawaje hakuna aliyepata kusikia malumbano hayo. Madsam hakuishia hapo, kesho yake alimuita mwanae Juma na kumueleza juu ya jambolile. Juma baada ya kupata taarifa hizo alisema"Mama mimwenyewe kunakitu kilinishangaza sana mpaka leo siwezi amini" "kitugani tena mwanangu?" mama alimuluza. Juma alimjibu"Sikuile muliyokuwa muna mpeleka Amina hospitalini, sikuweza amini machoyangu kuona mwili wa mtu kutokutoa kivuli haliyakuwa jua lina muangazia". Mama alidakia "nini..!? mbona hukunyambia mapema.?" "Nilipitiwa mama" Juma alimjibu huku akikuna kichwa. Kimya kilitanda kwa muda. Mara Juma akasema "mama unaonaje tukienda kwa wataalam?" "kufanya nini?" mama maye aliuza hukuakiwa kamkazia jicho. Juma akasema "watufafanulie juu ya jambo hili" "Nitangalia" mama alimjibu huku akiondoka zake.
Nisiku ya pili B.fatma hajafukia kichwakile tangu akabidhiwe, hivyo kilianza kuharibika na kutoa harufu kiasi. Mzee Ally(mumewe B.fatma) Alijisemea "nahisi kunamnyama kafia humundani, sijui paka huyo..! ilamufanye hadi kesho uweumeshatoka mzoga wake"
Siku ya pili yake. Madsam alikatashauri hivyo alimwambia mwanaye Juma waelekee hukokwa mganga kupata ufumbuzi waswalalao. Asubuhi majira ya saa5, baada yakumaliza shughuli za pale nyumbani, Madsam na mwanaye Juma waliekekea kwamganga katika kijiji chapili (kisangara) ingawaje hakuna aliyejua mtokoule kwani Nasibu hakuwaradhi na suala lawaganga.
Walipowadia kwamganga wakakaribishwa kwenye mkeka. Mganga akawambia "semeni shidayenu iliyo waleta" Madsam alielezea mkasamzima uliomkuta mwanaye Amina kabla ya kufariki. Mganga alicheka kwa sauti ya mnato"ha ha ha ha.." akawa kama nimwenye kuwakejeli, kisha akawaeleza "kunamengi ambayo hamuyajui, nduguyenu hajafa kiroho.." wote walitahamaki "Nini..! Unasemaje?" mganga akawambia "tulizeni munkari leo mtapata kujua yote yaliyojificha, nihivi nduyenu amekufa mwilitu haliyakua rohoyake ingalihai, nahata hivyo mwiliwake ulishaliwa nyama naistoshe kunamabaki ya viungo vya mwiliwake nyumbani kwenu. "naulemwili tuouzika je?" Madsam akiuliza huku akiwa na wasiwasi. Kabla hajajibiwa Juma naye alidakia "vipi kuhusu hiyo roho uliyosema ingalihai hadisasa?" mganga aliwambia "musijali nitawaeleza. Mwili wa ndugu yenu ulifufuliwa pale mulipo uzika, hivyo kwenye kaburi lake hakuna kituchochote na hiyo rohoyake imetundikwa katika mbuyu uliopo pale kijijini kwenu hatahivyo haitakuwa rahisi kuiona roho yake.
Baada ya maongezi marefu. Madsam alimuliza mganga "ninani anayefanya mambo haya?" mganga alimwambia "mutamjuatu mbaya wenu mukirudi nyumbani kwenu ilanitawapa dawa itakayowapa uwezo wa kugundua vilipo hifadhiwa viungomva mwili wa ndungu yenu, halikadhalika mbayawenu. Juma alimuliza mganga "tutamjuaje mbayawawetu?" "swalizuli kijana" mgana alijibu utamtambua kwakumtanzama usoni ataonekama nimwenyeaibu. Chukueni dawa hinzi mutazinyunyizia kuizunguka nyumba yenu sawa. Kwapamoja walitikia "ndiyo" mgana aliwapatia dawa nakisha wakarejea nyumbani kwao.
Walipofika nyumbanikwao majira ya sasa 8 mchana, hawakutaka kupoteza muda. Madsam alichukuwa dawaile aliyopewa nakuanza kuinyunyiza kuzunguka nyumba yao, hakutaka maongezi na mtu japokuwa mumewe alikuwa akimuliza "wewe unafanyanini..? Kwanza umetoka wapi?" Madsam hakumjibu lolote chazaidi alimwangalia hukuakiwa amemkunjiauso nawenye hasira. Nasibu alibaki akimshanga mkewe hakujua kilichokuwa kinaendeleya.
Pundesipunde B.fatma alitokandani nakusima mlangoni. Nibaada ya kuchefuliwa na harufu ya dawa iliyomwangwa pale nje, usokwau machoyake yaligongana na macho ya Juma
Mzee Ally aliporejea nyumbani toka kwenye mgahawa, aliwakuta Juma na bibi yake wanaangaliana kamawatu wenyekisasi, akawauliza "nyiye vipi mbona mnashangaana?" hakutaka kusubiri kupewa jibu laswali alilouliza, alimgeukia Juma nakumueleza "hivi wewe jana sinilikwambia utoe huomzoga unaonuka humondani?" Juma alimjibu "ndiyo babu, naendakuutoa sasa hivi" "harakisha..!" babu alimwambia hukuakiwa anakachini kwenye kitichake. Wakati huohuo Nasibu na mkewe walitokea nyuma yanyumba hukuwakiwa wanajibizana. Juma akiwa anaelekea ndani kufanya alichoagizwa na babu yake. B.fatma akiwa bado kasimama pale mlangoni mara nguvu zikamwishia, mwiliulitweta, kijasho chembamba kikaanza kumtiririka mashavuni huku akitetemeka kama kamwagiwa maji ya baridi, macho yake aliyainamisha chini. Moyoni alianza kujilaumu "uvivu wangu umeniponza launingali kifukia kichakile mapema yasingenikuta yote haya, leo nisikuyangu ya kudhalika" Wenzake walimshanga kwa haliile. Juma alipo ukaribia mlango, B.fatma alimzuia kuingia ndani kwa kumuwekea mkono kifuani kwake. Mzee Ally na Nasibu hawakujua kichokuwa kinaendelea, Madsam na Juma waliangaliana kwaishara ya kuligundua jambo fulani. B.fatma kwaaibu alikimbilia ndani nakujifungia mlango. Mzee Ally alimshanga "haaaa..! amechanganyikiwa au vipi?" kisha akawauliza wenzake "kwani kunatatizo gani?" Madsam bilakusita alimsimulia mkasa mzima. Mzee Ally alibaki mdomo wazi hakuamini alichokisikia. Nasibu baada ya kusikia yotehayo alipanda na hasira. Akauvamia mlango nakuanza kuungonga kwanguvu. B.fatma kulendani alishindwa kuvumilia nakuangua kilio.
Mayowe yalipoendelea kuzidi, majirani na wapitanjia walisogea enoelile. Wengiwao walidadisi "kwani kunanini hapa?" baadhi walipata fununu, wengine wakajizushia mambo wenye, eti hoo.! "ameuwamtu", wengine "anatakakujiuwa" wengine "mchawi" basi ikawa tafrani hakuna taarifa iliyoeleweka katiyao. B.fatma kulenda baada yakujua kunaumati mkubwa wa watu pole nje, aliacha kulia ilamapigo ya moyo yalienda mbiyo. Alipogeuza macho pombeni yake alikiona kisu... akakifuata nakukitwaa kisukile, hakuwa najinsi aliweka uwoga pembeni na kufumba macho huku akiwa anaielekeza ncha ya kisuki kwenye moyo wake, kwaharaka alikimbia na kujibamiza ukutani nakile kisu. Kisu kulingana kilichongoka sana, kilipenya katiya mbavu mbili hatimaye kuutoboa moyo, hapohapo moyo ukasimama kudunda. Kulenje watu waliokuwa karibu na mlango walikaa kimya baada ya kusikia sautikali iliyotoka ndani ikiambatana na kishindo kikubwa. Minong'ono ilififia hatimaye kimya kikatanda, marawaka msikia mtu anakorofuka mlendani.
Majirani wawili walimsaidia Nasibu kuvunja mlango. Waliupiga vikumbo vitatu tu, hatimaye walifanikiwa kuuvunja, wakamkuta B.fatma kesha fariki dunia kutokana na kupoteza damu nyingi. Nje kilammoja alitaka kushuhudia kilichotokea ikawa ni vurugu patashika. Wengine walilia wengine walisikitika nakuhuzunika. Juma alingia ndani nakutafuta vileviungo alivyo ambiwa na mganga kuwavimo nyumbani kwao, hatimaye alikiona kichwa cha marehemu Amina uvunguni mwakitanda, kwa ujasiri alikichukua, bila ya kujielewa alitokanacho nje. Madsam alipokionatu akiazimia Nasibu alibaki akibubujika machozi. Watu wengine wenye mioyo dhaifu walizimia wengine kilammoja alitafuta njia yake, ikawa ni kukanyangana. Asha alilia mpaka naye akapoteza fahamu. Baadhi ya wanaume walio salia eneoile walichukuwa kichwa na mwiliule na kuvihifadhi pamoja.
Kisha kuendelea na shughuli za mazishi.
Kesho yake kilekichwa kikazikwa kwenye kaburi lilelile la Amina.
.....MWISHO.
No comments