Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini Ya Pilipili Mbichi

Share:



Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama
Nyama ya ng’ombe vipande vidogo - 2lb            
Nyanya - 1
Kitunguu Kilichoktwa katwa - 1
Mafuta - 2 vijiko vya supu
Paprika (bizari ya masala ya rangi) - ½ kijiko cha chai
Kidonge cha supu - 1
Chumvi - Kiasi
Ndimu - Kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha nyama kwa chungio ili itoke maji. Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwerangi ya hudhurungi.
Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.
Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.

Vipimo Vya Mboga
Mchicha ulio katwa katwa                                  400 gm
Nyanya                                                            1
Kitunguu kilicho katwa                                      1
Nazi ya unga                                                     kiasi
Pilipili mbichi                                                     2
Mafuta                                                              ½ kijiko cha supu
Chumvi                                                              kiasi

Namna Ya Kutayarisha na Kupika
Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.
Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.
Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji
Tia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa
tayari kuliwa



Vipimo Vya Maharage
Maharage - 1 kopo
Kitunguu - 1
Nazi - 1 mug
Nyanya (itowe maganda) - 1 kiasi
Pilipili mbichi - 2
Mafuta - 1 kijiko cha supu
Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na kupika
Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.
kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.
Tia chumvi, maharage na nazi uwachie
moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.
Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi
Pilipili mbichi - 4/5
Kotmiri - 1 Kijiko cha supu
Ndimu - kiasi
Kitunguu saumu(thomu/galic) - 1 chembe
Mafuta ya zaituni - 2 vijiko Vya supu
Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha
Kwenye blender, tia vipimo vyote na sage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.

Vipimo Vya ugali
Maji - 4   Vikombe  kiasi inategemea na unga
Unga wa sembe - 2   vikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri.
Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.


No comments